ALIYEKUWA MDHAMINI WA YANGA YUSUPH MANJI AFARIKI DUNIA

Uongozi wa timu ya Yanga Yenye makao makuu yake Jangwani Dar es salam, kupitia mitandao yao ya kijamii umetoa taarifa ya Kupokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha aliyekuwa mdhamini na Mwenyekiti wa timu hiyo maarufu kama Yusuph Manji

Kwa Mujibu wa taarifa iliyotolewa na club hiyo inasema kuwa kifo cha Manji kimetokea hii leo 30 June, 2024 katika nchi ya Marekani ambapo Alikuwa akipatiwa matibabu ya maradhi yaliokuwa yanamsumbua


Kwa Mujibu wa Eng. Hersi Said ambaye ni Rais wa Yanga kwasasa amemtaja Manji kama kiongozi hodari na mahiri aliyejituma na kujitoa kwaajili ya maendeleo ya timu yao, na kusema kuwa kifo chake ni pigo kwa wanayanga na familia nzima ya michezo

“Manji alihudumu katika nafasi Mbalimbali za kiungozi ndani ya club yetu kama mdhamini na Mwenyekiti ambapo hadi umauti unamkuta alikuwa mwanachama na Young Africans Sports Club, uongozi wa Young Africans Sports Club unatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na wanamichezo wote nchini kwa msiba mzito wa mpendwa wetu”



Post a Comment

Previous Post Next Post