MIL. 800 YAKUSANYWA KWENYE HARAMBEE, KKKT DAYOSISI YA KATI

Kupitia harambee iliofanyika june 30, 2024 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya kati Singida takribani kiasi cha sh. milioni 800 zimekusanywa ikiwa ni ziada ya milioni 100 kutoka kwenye kiasi kilichotarajiwa

Katika harambee hii ya pili iliyokusudiwa kukusanya kiasi cha milioni 700 ziada ya milioni 300 kutoka kwenye harambee ya mwaka jana iliyokusanya kiasi cha milioni 400 kwa lengo la kwenda kuimarisha vituo vya afya, shule na mfuko wa utumishi



Akizungumza kwaniaba ya mgeni rasmi, Prof. Kitila Mkumbo amewataka wananchi wawe na desturi ya kujitolea ili waongezewe zaidi kama ambavyo maandiko yanasema

Kwa mujibu wa askofu Dr. Syprian Hilinti amesema harambee ya mwaka huu imekusudia kukusanya milioni 700 ili kwenda kuimarisha vituo vya elmu Ihanja na Kiomboi pamoja vituo vya afya Singida Mjini na Iyambi na kuinua mfuko wa utumishi

“Dayosisi yetu tumejiwekea nadhiri kwa mungu na patano kupitia vikao vya kimaamuzi na kikatiba kwamba kila mwaka kila msharika kuanzia mtoto hadi mzee atamuwekea mungu alama kwa mchango wake wa sadaka ya hiari na moyo wa kupenda kama mungu anavyomuongoza”

Kwa upande wake mkuu wa kanisa Tanzania Alex Malasula amewataka vijana nchini kujielekeza maisha yao kwa mungu ili kudumisha amani kwani amesema endapo vijana wakijielekeza kwa mungu chochote atakachokifanya atamuuliza mungu kabla ya kutenda hivyo nchi itakuwa mahali amani

“kijana akiweka maisha yake kwa mungu nchi yetu itakuwa mahali pa amani, nchi yetu itakuwa mahali penye ufahamu, kijana aliyeweka maisha yake mahali pa mungu anaufahamu kabla hata ya kuamua lolote anamuuliza mungu”

Katika harambee hio imehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka madhehebu tofauti ya dini tofauti, viongozi wa serikali ngazi tofauti, viongozi wa vyama vya siasa, wabunge mbalimbali wa mkoa wa Singida, huku mgeni rasmi akiwa waziri wa fedha Dr. Mwigulu Nchemba akiwakilishwa na waziri wa mipango na uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo

Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego amesema serikali ya mkoa wa Singida inaushirikiano mzuri na madhehebu ya dini katika kuendeleza maendeleo ya mkoa na ndiomana tukio hilo la kikanisa limejumuisha watu wa hadhi na imani tofauti

“Na hizifedha zinazochangwa zinaenda kutoa mchango mkubwa kwenye elimu na afya, kila mmoja wetu ataguswa moja kwa moja kupitia ndugu yake, mdogo wake, kakayake, rafikiyake, mtoto yake au mgeni wake, kwahiyo hili jambo ndugu zangu ni lakwetu sote” alisema





 

Post a Comment

Previous Post Next Post