STEVE MUKWALA NA TUMAINI JIPYA LA MSIMBAZI

Ni mshambuliaji raia kutoka nchini Uganda, aliyejiunga rasmi msimbazi kuwafuta machozi ya muda mrefu mashabiki na wanachama wa Simba kwenye ule mfupa uliowashinda baadhi ya washambuliaji kwa miaka ya hivi karibuni wakiwemo kina Jeneral Mosses Phiri, na Jean Baleke,

Steve Mukwala mwenye umri wa 20 na Minne, mshambuliaji kinara aliyefunga mabao 14 na usaidizi wa magoli mawili katika michezo 28 akiwa na Asante Kotoko ya nchini Ghana msimu uliomalizika, anasaini miaka 3 kuitumikia nembo ya Simba

Ni Mukwala Mwenye urefu wa futi 5.9 amebeba matumaini ya wanamsimbazi kutibu moja ya eneo lililokuwa na mapungufu makubwa msimu uliomaliza katika kikosi hiko, eneo la safu ya ushambuliaji, anakuja kuungana na Fredy Michael kuiongoza safu hio

Steve Mukwala katika historia yake ya kabumbu amevitumikia vilabu kadhaa nchini Uganda ikiwemo Vipers Fc, Maroons Fc kabla ya kutimkia Asante Kotoko ya nchini Ghana

Licha ya kufunga magoli 14 msimu uliopita, msimu wa mwaka juzi alipachika magoli 11 pekee katika michezo 31 aliyocheza ya ligi

Siku moja kabla ya kutambulishwa Mukwala pale msimbazi, alitambulishwa mchezaji raia wa Zambia Joshua mwana wa Mutale, kiungo mwenye umri wa miaka 22 aliyejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka 3 akitokea Power Dynamo ya nchini Zambia

Ni Joshua Mutale anayeweza kucheza akitokea kulia, kushoto ama kucheza nyuma ya mshambuliaji kama namba 10

Mutale Akiwa Zambia na Power Dynamo msimu uliopita amefunga magoli 8  katika michezo 26 aliyocheza

Mpaka sasa  simba imeshatambulisha wachezaji 3 waliowasajili katika kikosi chao nje na walioongezewa mkataba. Mapema kabisa alitambulishwa Lameck Lawi kutoko kwa wanamangushi, Costal Union ya mkoani Tanga anayecheza nafasi ya mlinzi wa kati, kisha kiungo Joshua Mutale na baadae mshambuliaji Steve Mukwala


https://www.youtube.com/watch?v=tfBxPHupinc


Post a Comment

Previous Post Next Post